NGUMI KUPIGWA MEI 16 BAGAMOYO MJINI

Na Mwandishi Wetu 

MPAMBANO mkali wa masumbwi utafanyika Bagamoyo Mei 16 katika ukumbi wa  che kwa che uliopo Bagamoyo mjini mpambano uho utawakutanisha bondia Iddi Pialali wa Kiwangwa Bagamoyo atakaezipiga na Adam Ngange wa Chanika Dar es salaam

mpambano uho utachezwa baada ya kila bondia kujigamba kuwa yeye ni zaidi ya mwenzie siku hiyo pia kutakuwa na mapambano ya utangulizi yatakayowakutanisha mabondia mbalimbali wenye upinzani mkali katika masumbwi

Rashidi Haruna atakumbana na Kaminja Ramadhani na Harid Hongo atakabiliana na Kishoki Mbishi mpambano mwingine ni Abdallah Samata atakaye zidunda na Maono Alli 

mipambano hiyo inaletwa kwenu na Sharif Promotion wakati mgeni rasmi siku hiyo ni bondia kutoka morogoro Cosmas Cheka ambaye atakuja kuwapa nasaa mbalimbali mabondia na mashabiki wa mchezo wa masumbwi kuweza kusonga mbele kwa mchezo uho mjini Bagamoyo

kingilia katika mpambano uho ni Tsh, 8000 kwa V.I.P na kwaida ni sh. 5000

Katika mpambano huo siku hiyo kutakuwa na upatikanaji wa DVD za mafunzo ya mchezo wa ngumi  kali pamoja na kutambua sheria zake zikiwa na mabondia wakali kama vile
Floyd Mayweathar vs Manny Paquaio 2015 , Saul 'canelo' alverez ,Mike Tyson,Mohamed Ali,Ferex Trinidad,Miguel Cotto na wengine wengi

pia kuta kuwa na vifaa vya mchezo vitakaokuwa vikigawiwa na kocha  Rajabu Mhamila 'Super D' kwa mabondia watakaofanya vizuri siku hiyo na vingine kuuzwa kwa galama nafuu na kocha huyo kwa ajili ya kuamasisha mchezo wa masumbwi nchini
Share on Google Plus

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment

0 comments:

Inaendeshwa na Blogger.

Wanaofuata

TANGAZO

My Blog List