WACHA TUFE LAKINI USHINDI LAZIMA,NAPE APATA AJALI YA GARI

KATIBU wa Itikadi na Uenezi wa Chama cha Mapinduzi (CCM), Nape Nnauye amepata ajali mbaya akiwa njiani kuelekea Lindi akitokea jijini Dar es Salaam.

Nape amenusurika kifo katika ajali hiyo iliyotokea leo asubuhi katika eneo la Njia Nne Kilwa akiwa anatoka Dar kuelekea jimboni kwake.

Nape ambaye pia ni mgombea Ubunge wa Jimbo la Mtama, Lindi alipata ajali hiyo baada ya tairi la mbele la gari aliyokuwa akiendesha aina ya Toyota Land Cruiser kupasuka na kupinduka mara kadhaa katika eneo la Nyangao mkoani Lindi.

Katika gari hilo, Nape alikuwa peke yake na ndiye alikuwa akiendesha gari hilo ambapo amepata majeraha madogo ila anaendelea vizuri.

Akizungumza na mtandao huu, Nape amesema: "Namshukuru Mungu nimetoka salama na nawaomba wananchi wasiwe na hofu japo ajali ilikuwa mbaya maana gari lilipinduka mara kadhaa, nimepata majeraha madogomadogo na michubuko ila ni mzima.

Gari limeharibika vibaya ila ninachoshukuru nilikuwa nimefunga mkanda na 'air bag' nazo zimenisaidia." 

Kabla ya ajali hiyo, Nape alikuwa jijini Dar es Salaam ambapo aliungana na mgombea urais kwa tiketi ya CCM, Dk. John Pombe Magufuli aliyekuwa na mikutano kadhaa ya kampeni katika jiji la Dar na baada ya shughuli hiyo alikuwa akirejea Lindi kuendelea na kampeni kwenye jimbo lake la Mtama.

Name:  IMG-20151022-WA0006.jpg
Views: 57021
Size:  86.4 KB
Name:  IMG-20151022-WA0004.jpg
Views: 44314
Size:  80.5 KB
Name:  IMG-20151022-WA0005.jpg
Views: 42390
Size:  51.8 KB
Share on Google Plus

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment

0 comments:

Inaendeshwa na Blogger.

Wanaofuata

TANGAZO

My Blog List