Mkuu wa Wilaya ya Temeke Sophia Mjema amepokea msaada wa mifuko 600 ya cement kutoka kwa Shirika lisilo la kiserikali

Mkuu wa Wilaya ya Temeke Sophia Mjema amepokea msaada wa mifuko 600 ya cement,na ahadi ya Madawati MIA nne(400),kutoka kwa Shirika lisilo la kiserikali la SGM foundation yenye thamani ya zaidi ya Shilingi milioni 6 kwa ajili ya shule ya msingi Mbande. kwa lengo la kuongeza Madarasa na Ujenzi wa Uzio.
Mwenyekiti wa Kamati ya Wazazi ya shule ya msingi Mbande - Martin Jairo,amepokea na kushukuru kwa msaada huo. Pia amewataka Wazazi wafuatilie mwenendo wa watoto  wao,ili wapate elimu iliyo bora itakayo changia katika maendeleo yao ya shule. pia amezungumzia suala la wanafunzi kujihusisha katika makundi hatarishi.
Mkuu wa Shule ya Mbande-Dauden mwakyambiki na Afisa elimu kata ya Chamazi-Balbina Ngalaba wameshukuru kwa msaada  uliotolewa na kuwataka Wazazi, wanafunzi  na Walimu  kushirikiana ili kupata elimu iliyo bora.

Share on Google Plus

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment

0 comments:

Inaendeshwa na Blogger.

Wanaofuata

TANGAZO

My Blog List