KIGAMBONI UVAMIZI WA ARDHI BASI

Mkurugenzi wa Manispaa ya Kigamboni Stephen Katemba ametoa wiki moja kwa watu wote wenye Mashamba Pori kuwasilisha Mpango kazi wa maeneo wanayomiliki, huku akiwataka wavamizi wa maeneo ya Serikali kuondoka mara moja kabla ya sheria kuchukua  Mkondo wake. Aidha amewataka Wenyeviti wa Serikali za Mitaa na Watendaji kufanya kazi kwa uwadilifu na kutoa onyo kwa Watumishi hao kwa kuwataka kumaliza mgogoro ya ardhi ambayo idadi yake sasa inafikia 217.  Mkurugenzi huyo amesema hatakuwa tayari kutumia kiasi cha Shilingi bilioni 4  kwa ajili ya kununua eneo la Ujenzi wa Ofisi za Manispaa hiyo kwa kuwa yako maeneo yanayptosheleza  Ujenzi huo,  yaliyotengwa tangu enzi ya Baba wa Taifa Hayati Mwalimu Julias Kambarage Nyerere. Pia ameeleza mkakati wake wa kufufua Kisima Kikubwa  kilichochimbwa enzi za Mwalimu Nyerere  kilichokuwa na uwezo mkubwa wa kusambaza Maji safi na salama maeneo ya Kigamboni.    Diwani wa Kata ya Somangila Kigamboni Frances Masanja Chichi pamoja na Viongozi wa mtaa wa Mbwamaji wamesema wapo tayari kushirikiana na Mkurugenzi huyo kutatua kero zilizopo ili waweze kuleta maendeleo. Zoezi la ukaguzi wa eneo lililopo mtaa Mbwamaji ambalo linalokusudiwa kujengwa Halmashauri ya Kigamboni, zoezi ambalo limeenda sambamba na Usafi wa Mazingira.

Share on Google Plus

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment

0 comments:

Inaendeshwa na Blogger.

Wanaofuata

TANGAZO

My Blog List