Jeshi la polisi wilaya ya bagamoyo mkoa wa Pwani limedaiwa kuwaua Vijana wawili wa familia moja ya jamii ya wafugaji.Vijana hao wameuwawa na askali polisi wa wilaya ya BAGAMOYO katika kijiji cha Kidomlole kata ya Fukayosi mkoani PWANI baada ya kuhitaji kuhesabu mifugo yao ambayo askari hao walitaka kuichukuwa bila kuhesabiwa kwa kile kinachodaiwa ni zoezi la kuwaondoa wafugaji walioingia wilayani humo kinyume na taratibu.
Baadhi ya wafugaji wakizungumza baada ya uongozi wa chama cha wafugaji tanzania na jeshi la polisi kufika katika eneo hilo wameeleza,
MELIKUTA KAMBALELEGA akielezea jinsi hali ilivyotokea na kupata majeruhi. Huku YOHANA ROGER na baba mzazi wa watoto hao kambalelega Gisamoda walielezea pia hali ya tukio zima lilivyokuwa.
Hata hivyo baada ya kutokea mauji hayo mwishoni mwa mwezi wa pili mwaka huu jamii hiyo yawafugaji ilipiga kambi katika eneo hilo yalipofanyika mauaji na kudai kutokukubali kuondoa miili ya vijana hao kuifadhiwa lakini jitihada za kiongozi wa chama cha wafugaji Tanzania BWANA MAGEMBE MAKOYE na Wazee wa kimila wa eneo hili wakatumia busara kuwaomba wafugaji hao kuwa wavumilifu huku taratibu zikifuata ili kuwachukulia hatua waliofanya tukio hilo.
Alhaj MAJID MWANGA ni mkuu wa wilaya ya Bagamoyo na mwenyeiti wa kamati ya ulizi na usalama ya wilaya hiyo je anazungumziaje tukio hilo?
Ni miezi 6 sasa tangu kutokea kwa mauji ya mmoja wawafugaji katika kijiji cha makurunge na hili ni tukio llingine ambao limedaiwa kufanya na askari polisi wa wilaya hiyo hata hivyo miili ya vijana hao imechukuliwa chini ya ulinzi wa jeshi la polisi imehifadhiwa katika hosptali ya wilaya bagamoyo kwa uchunguzi zaidi na walifariki SAINGA KAMBALELEGA na LUMAYE KAMALELEGA.
- Blogger Comment
Jisajili kwenye:
Chapisha Maoni
(
Atom
)
Inaendeshwa na Blogger.
About Me
Wanaofuata
TANGAZO
My Blog List
-
-
SUPER D AMUANDAA SUNDAY KIWALE KWA USHINDI WA K,O JANUARY 31 TANGA ATAKAPOZIPIGA NA YOHANA MCHANJA - SUPER D AMUANDAA SUNDAY KIWALE KWA USHINDI WA K,O JANUARY 31 TANGA ATAKAPOZIPIGA NA YOHANA MCHANJA Na Mwandishi Wetu KOCHA wa kimataifa wa mchezo wa masum...Miaka 5 iliyopita
-
SUPER D AMUANDAA SUNDAY KIWALE KWA USHINDI WA K,O JANUARY 31 TANGA ATAKAPOZIPIGA NA YOHANA MCHANJA - Na Mwandishi Wetu KOCHA wa kimataifa wa mchezo wa masumbwi nchini Rajabu Mhamila 'Super D' ambaye kwa sasa anamnowa bondia Sunday Kiwale 'Moro Best' kwa aj...Miaka 5 iliyopita
-
BONDIA MAKUBI ATAMBA KUMPIGA ABDALLAH MA MOROGORO OKTOBA 4 KATIKA UKUMBI WA 361 MWENGE - Na Mwandishi wetu Bondia Ibrahim Makubi yupo kambini kwa ajili ya mazoezi yake ya kumkabili bondia abdallah kingolwira wa ( morogoro ) katika pambano l...Miaka 5 iliyopita
-
JUMA CHOKI AJIANDAA NA MASHINDANO YA KING OF THE RING JULAI 28 - Bondia Ibrahimu Makubi kushoto akioneshana umwamba na Juma Choki wakati wa Mazoezi yanayoendelea katika kambi ya Super D iliyopo shule ya Uhuru Kariakoo...Miaka 6 iliyopita
-
0 comments:
Chapisha Maoni