JESHI LA POLISI WILAYA YA BAGAMOYO LIMEDAIWA KUWAUA VIJANA WAWILI.

Jeshi la polisi wilaya ya bagamoyo mkoa  wa Pwani limedaiwa kuwaua Vijana wawili  wa familia moja ya jamii ya wafugaji.Vijana hao wameuwawa na askali polisi wa wilaya ya BAGAMOYO  katika  kijiji cha Kidomlole kata ya Fukayosi  mkoani PWANI  baada ya kuhitaji  kuhesabu mifugo yao ambayo askari hao walitaka kuichukuwa  bila kuhesabiwa   kwa kile kinachodaiwa ni zoezi la kuwaondoa wafugaji walioingia wilayani humo kinyume na taratibu.
Baadhi ya wafugaji wakizungumza baada ya uongozi wa chama cha wafugaji tanzania na jeshi la polisi kufika katika eneo hilo wameeleza,
MELIKUTA KAMBALELEGA akielezea jinsi hali ilivyotokea na kupata majeruhi. Huku YOHANA ROGER  na baba mzazi wa watoto hao kambalelega  Gisamoda walielezea pia hali ya tukio zima lilivyokuwa.
Hata hivyo baada ya kutokea mauji hayo mwishoni mwa mwezi wa pili mwaka huu jamii hiyo yawafugaji ilipiga kambi katika eneo hilo yalipofanyika mauaji na kudai kutokukubali kuondoa miili ya vijana hao kuifadhiwa lakini jitihada za kiongozi wa chama cha wafugaji Tanzania BWANA MAGEMBE MAKOYE na Wazee wa kimila wa eneo hili wakatumia busara kuwaomba wafugaji hao kuwa wavumilifu  huku taratibu zikifuata ili kuwachukulia hatua waliofanya tukio hilo.
Alhaj MAJID MWANGA ni mkuu wa wilaya ya Bagamoyo na mwenyeiti wa kamati ya ulizi na usalama ya wilaya hiyo je anazungumziaje tukio hilo?
Ni miezi 6 sasa tangu kutokea kwa mauji ya mmoja wawafugaji  katika kijiji cha makurunge na hili ni tukio llingine ambao limedaiwa kufanya na askari polisi wa wilaya hiyo hata hivyo miili ya vijana  hao  imechukuliwa  chini ya ulinzi wa jeshi la polisi imehifadhiwa katika hosptali ya wilaya bagamoyo kwa uchunguzi zaidi na walifariki  SAINGA KAMBALELEGA na LUMAYE KAMALELEGA.

Share on Google Plus

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment

0 comments:

Inaendeshwa na Blogger.

Wanaofuata

TANGAZO

My Blog List