Ikiwa leo ni siku ya maadhimisho ya uhuru wa vyombo vya habari, Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Dk. Harrison Mwakyembe ameagiza vituo vya redio na runinga nchini kusoma vichwa vya habari tu vya magazeti kuanzia kesho.
Dk. Mwakyembe ameyasema hayo leo alipokuwa akitoa ‘neno’ kama mgeni rasmi katika maadhimisho hayo jijini Mwanza. Amesema kuwa kwa kusoma vichwa vya habari tu, wananchi watakuwa na hamu ya kutaka kuyasoma magazeti kupata habari kamili. Hivyo, watanunua.
Waziri Mwakyembe pia amewahakikishia waandishi wa habari kuwa Serikali itaendelea kulinda haki na uhuru wa vyombo vya habari ikiwa ni pamoja na kutoa ulinzi kwa waandishi wa habari za uchunguzi.
Katika hatua nyingine, ameahidi kuwa wizara yake kupitia Idara ya Habari Maelezo itahakikisha waandishi wa habari wanapewa ushirikiano wa kutosha wanapohitaji taarifa kutoka Serikalini.
Amesema kuwa wizara yake itaweka utaratibu wa kukutana na waandishi wa habari kila mwezi ili kujadili changamoto wanazopitia katika kupata habari kutoka kwa vyanzo vya Serikali.
Home / gloria media
/ Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Dk. Harrison Mwakyembe ameagiza vituo vya redio na runinga nchini kusoma vichwa vya habari tu vya magazeti kuanzia kesho.
- Blogger Comment
Jisajili kwenye:
Chapisha Maoni
(
Atom
)
Inaendeshwa na Blogger.
About Me
Wanaofuata
TANGAZO
My Blog List
-
-
SUPER D AMUANDAA SUNDAY KIWALE KWA USHINDI WA K,O JANUARY 31 TANGA ATAKAPOZIPIGA NA YOHANA MCHANJA - SUPER D AMUANDAA SUNDAY KIWALE KWA USHINDI WA K,O JANUARY 31 TANGA ATAKAPOZIPIGA NA YOHANA MCHANJA Na Mwandishi Wetu KOCHA wa kimataifa wa mchezo wa masum...Miaka 5 iliyopita
-
SUPER D AMUANDAA SUNDAY KIWALE KWA USHINDI WA K,O JANUARY 31 TANGA ATAKAPOZIPIGA NA YOHANA MCHANJA - Na Mwandishi Wetu KOCHA wa kimataifa wa mchezo wa masumbwi nchini Rajabu Mhamila 'Super D' ambaye kwa sasa anamnowa bondia Sunday Kiwale 'Moro Best' kwa aj...Miaka 5 iliyopita
-
BONDIA MAKUBI ATAMBA KUMPIGA ABDALLAH MA MOROGORO OKTOBA 4 KATIKA UKUMBI WA 361 MWENGE - Na Mwandishi wetu Bondia Ibrahim Makubi yupo kambini kwa ajili ya mazoezi yake ya kumkabili bondia abdallah kingolwira wa ( morogoro ) katika pambano l...Miaka 5 iliyopita
-
JUMA CHOKI AJIANDAA NA MASHINDANO YA KING OF THE RING JULAI 28 - Bondia Ibrahimu Makubi kushoto akioneshana umwamba na Juma Choki wakati wa Mazoezi yanayoendelea katika kambi ya Super D iliyopo shule ya Uhuru Kariakoo...Miaka 6 iliyopita
-
0 comments:
Chapisha Maoni