Pamoja na juhudi zinazofanywa na Serikali za kukomesha mauaji lakini hali inaonekana kuwa bado tete Wilayani Kibiti mkoani Pwani baada ya viongozi wengine wawili kupigwa risasi usiku wa kuamkia leo.
Viongozi waliopigwa risasi ni Mtendaji wa Kijiji cha Mangwi kilichopo katika Kata ya Mchukwi, Shamte Makawa na Mwenyekiti wa Kitongoji cha Mangwi, Maiko Nicholaus.
Aidha, Kamanda wa Jeshi la Polisi Mkoani Pwani, Onesmo Lyanga amekiri kutokea kwa tukio hilo na kusema kuwa upelelezi unaendelea ili kuwabaini wale waliohusika katika tukio hilo.
Hata hivyo, watu 37 wameuawa tangu vitendo hivyo vianze katika Wilaya za Kibiti, Rufiji na Mkuranga mkoani Pwani wakiwemo askari 13.
MAMLAKA YA HALI YA HEWA DUNIANI KUENDELEA KUUNGA MKONO JITIHADA ZA TANZANIA
KUKABILIANA NA MAAFA
-
Katibu Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge, na Uratibu) Dkt. Jim Yonazi
akisalimiana na Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Hali ya Hewa Duniani Bi.
Celest...
Saa 1 iliyopita
0 comments:
Chapisha Maoni