GEREJI ENEO LA WAZI.



Gereji Eneo la wazi
Gloria Matola
16 Oktoba, 2017
Dar es salaam.

Wananchi wa Mtaa wa Msisiri B Manispaa ya Kinondoni Jijini Dar Es Salaam wameilalamikia Serikali kuruhusu matumizi ya eneo la wazi kujengwa Gereji isiyokuwa rasmi hali inayohatarisha usalama wa watoto wao kutokana na kuzagaa kwa vyuma chakavu.
Awali eneo hilo lilitengwa kama eneo la wazi lakini baadae alikabidhiwa Mfanyabiashara Charles Kombe kwa makubaliano ya kuijengea ofisi Serikali ya Mtaa na yeye kuruhusiwa kutumia eneo hilo kufyatua matofali ya saruji.

Matumizi ya awali ya eneo hilo yakabadilika kwa Mfanyabiashara huyo kufungua Gereji hali iliyowalazimu wananchi hao kupaza sauti zao.

Kutokana na Malalamiko hayo Star tv ilibisha hodi ofisi ya Serikali ya Mtaa huo na kukutana na Mwenyekiti aliyethibitisha kumuita mfanyabiashara huyo mara kadhaa bila mafanikio huku akidai hautambui uongozi huo.

Star Tv ilifika ofisini kwa mfanyabiashara huyo Charles Kombe maarufu kama Galilaya kutaka kujua ana lipi la kuzungumza kuhusiana na malalamiko haya

Galilaya alikiri kuwa alikabidhiwa eneo hilo na uongozi wa Serikali ya Mtaa ya wakati huo na kukataa kuzungumzia malalamiko hayo kwa kile alichodai kuna kesi mahakamani kuhusiana na eneo hilo huku akikataa kurekodiwa.

Star Tv ilikwenda mbali zaidi na kumtafuta Mkuu wa Idara inayosimamia maeneo ya wazi Manispaa ya Kinondoni Dismas Hafidh ambaye naye alikataa kurekodiwa huku akidai mfanyabiashara huyo kuwa mkorofi.



Share on Google Plus

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment

0 comments:

Inaendeshwa na Blogger.

Wanaofuata

TANGAZO

My Blog List