KATA YA 14 TEMEKE WANAENDA NA MARIAM MTEMVU.



Mwenyeki wa UWT taifa Marry Chatanda akizindua kampeni ya Uchaguzi ya 14 Temeke wilaya ya Temeke jijini Dar es saalam amewaomba Wananchi ifikapo okotobar 29 2025 wawachague viongozi wa chama cha Mapinduzi Urais Ubunge Udiwani ili waweze pata maendeleo watakapo chagua Mafiga matatu

Akiongea katika Mkutano wa Adhara Uwanja wa Mapumba Temeke amesema mama Samia ni Mchapa kazi pia ameweza kufanikisha miradi mbalimbali ya maendeleo ikiwepo ujenzi wa Barabara Umeme Maji Shule Vituo vya Afya Masoko Madaraja na garimoshi (Treni) za Umeme mabasi ya Mwendo kasi ambapo hivi sasa kuna mradi wa Maji Kidunda mradi huo watanufaika mikoa miwili Pwani na Dar es salaam.


Mgombea Ubunge Jimbo la Temeke Mariamu Kisangi amesema wakimchagua ataibadilisha Temeke kuwa yenye kiwango atatekeleza miradi ya maendeleo Afya Elimu Miundombinu ya Barabara Umeme na Maji na kusimamia pesa za Mikopo isiyokuwa na Riba ya Manispaa kwa Vijana akina mama na Walemavu

Mgombea nafasi ya Udiwani kata Temeke 14 Marianu Mtemvu amesema akichaguliwa atasimamia vizuri fedha za mradi wa ujenzi wa Zahanati ya Temeke na watapunguza gharama za matibabu Kwenda mbali na makazi yao


Kampeni zikiendelea za uchaguzi Chama Tawala Ccm na Vyana vya upizani kila mmoja akijinadi kwa sifa za kuwatekelezea maendelo ya wananchi ya taifa.








Share on Google Plus

About SDM PRODUCTION MEDIA

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment

0 comments:

Inaendeshwa na Blogger.

Wanaofuata

TANGAZO

My Blog List