KIJICHI SANAA GROUP WATAFUTA MDHAMINI

KUNDI la sanaa la ngoma na maigizo, lenye jina la Kijichi Sanaa Group, kilichopo Kijichi wilaya ya Temeke jijini Dar es salaam wameiomba Serikali  iwasaidie  mtaji ili kufanikisha kurekodi kazi zao  za sanaa.
 
Kundi hilo lenye jumla ya vijana 24, linazaidi ya miaka saba na limeshapata usajili toka Baraza la Sanaa Tanzania (Basata) Septemba 23, 2011 kwa jina la Kijichi Sanaa Group, halijawahi kurekodi kutokana na kutokuwa na mtaji wa kutosha kufanikisha jambo hilo.
Msemaji wa kundi hilo, Ahmed Mshiraz aliomba serikali kusaidia vijana wanaojituma katika kazi za sanaa kwa kutumia vipaji walivyonavyo  ili kuondoa umaskini unaowazunguka.
Mshiraz aliongeza kuwa vijana wengi wamekata tamaa baada ya kukosa uwezeshwaji licha ya kujituma kwa uwezo wao wote kuonyesha vipaji vyao hali inayochangia vijana kijihusisha na vitendo viovu vikiwemo uporaji, matumizi ya dawa za kulevya, ubakaji, ushoga, usagaji na kazi haramu kama ujangiri.
Naye mwenyekiti wa kundi hilo, Maulid  Mbarouk ameiomba serikali na wadau wa maendeleo kujitokeza kusaidia mitaji, ili vijana hao waweze kutoa kazi walizonazo ambazo wanashindwa kuzitoa kutokana na kutokuwa na mtaji wa kuwawezesha kurekodi kazi hizo.
 
Mbarouk alisema alisema kundi ilo linajiushughulisha na sanaa za ngoma, filamu, uimbaji, mpira, mapishi pamoja na maswala ya manzingira ambapo hujitolea kufanya bure kwenye mitaa mbalimbali nchini.
Pia kundi hilo linaomba mtu yeyote mwenye uwezo wa kulizamini kundi hilo ajitokeze ili kuendeleza vipaji vya vijana hao na kuwawezesha kufikia malengo yao ikiwemo kurekodi kazi zao.
 
Share on Google Plus

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment

0 comments:

Inaendeshwa na Blogger.

Wanaofuata

TANGAZO

My Blog List