WAMAMA WA TABATA WAPATA MAFUNZO YA UJASIRIAMALI


JUMUIYA ya akina mama wasiojiweza kiuchumi   120 wanaoishi kata ya Tabata jijini Dar es salam wamepewa mafunzo ya mwezi mmoja ya Ujasiriamali ili kuwakomboa Kiuchumi.

Mafunzo haya yamejumuisha utengenezaji wa Batiki, Vikoi, utengenezaji wa mafuta, Sabuni na Usindikaji wa vyakula na matunda.

Akina mama hawa waliopewa mafunzo na Taasisi binafsi ya Tiba mbadala ya GHCHC wanakabiliwa na changamoto ya uhaba wa mitaji na upatikanaji wa soko la uhakika la bidhaa zao.

Umoja huo pia umewezeshwa na mtaji wa kianzio wa Sh 100,000 kutoka mfuko wa PSPF ambao unawapa mwanzo mpya.

Mratibu wa mafunzo hayo, Ferdinand Ngowi alisema wameamua kuunga mkono jitihada za Serikali za kuwakwamua wakinamama kiuchumi.

 
Share on Google Plus

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment

0 comments:

Inaendeshwa na Blogger.

Wanaofuata

TANGAZO

My Blog List