SHEKHE mkuu wa Mkoa
Dar es salaam Alhad Mussa Salum amewataka
Waislamu kote nchini kukihifadhi
Kitabu Kitukufu cha Quraan hatua itakayowapa Swawabu kwa Mwenyezi Mungu.
Ameyasema hayo hivi karibuni
katika viwanja vya Mwembe yanga jijini Dar es Salaam wakati akizindua
Tamasha la maonyesho ya miujiza ya Kitabu cha quraan kilicho hifadhiwa kwa kipindi
cha miaka 51.
Naye Hashimu Ramadhani amewataka waislamu kuachana na mambo
ya kidunia badala yake wafuate dini ya kiislamu inavyotaka kumcha na kumtumikia
mwenyezi mungu ili waweze kupata swawabu na masuala yao yatakuwa ya kheri na
yenye Baraka.
Osama Ismail ambaye alikuwa mshiriki katika tamasha hilo aliweza
kuonesha kipaji chake cha uwezo mkubwa
wa kusoma kitabu Quran.
Mbali na hayo kijana Mohamed Tagy Khany amewataka waislamu kuhifadhi
Quran kwa miaka 51 kwa kuwa ni vema waislamu kuchukua mafunzo yote ya kitabu
hicho an kufuata sheria za mungu.
0 comments:
Chapisha Maoni