WATANZANIA WATAKIWA KUNUNUA BIDHAA ZAO


Na  Gloria   Matola

JAMII ya Watanzania   nchini imeshauriwa kuthamini na kununua bidhaa zinazotengenezwa nchini ili kukuza soko la ndani  pamoja na kuongeza ajira kwa vijana ili kuwasaidia kujikwamua kiuchumi.


Hayo yameelezwa na mjasiriamali wa Bagamoyo Wine,Teddy Alban Davis ambaye ni  mwekezaji  mdogo wa mkoa wa Pwani wilaya ya Bagamoyo.

Teddy alisema changamoto kubwa anayokabiliwa nayo katika uwekezaji mdogo ni ukosefu wa uwakika  wa masoko ndani na nje kwa kuwa Watanzania hupenda kununua bidhaa za kutoka nje wakidhani ndio bora zaidi.                                              

Tedy alisema inatakiwa kuwe na ushirikiano kati ya Serikali na Wajasiriamali wa ndani ili kazi zao ziwez kuthaminika na kupata nafasi ya kuwepo katika maonyesho ya ndani, sabasaba, nanenane na kwenye maonyesho la soko la afrika mashariki bila kubaguliwa.

Pia alisema katika mwezi mtukufu wa Ramadhani biashara imekuwa ngumu kutokana na mkoa wa Pwani hususani wilaya ya agamoyo kuwa na waumini wengi wa dini ya kiislam ambao wengi wao ufunga ili kukamilisha moja ya nguzo tano za uislam.

Naye  Imamu mkuu wa Msjidi Ramiya, Maalim Simba Abuuqhari Ramiya amewataka  Waislam wote nchini kuheshimu mwezi wa Ramadhani  nakumtumikia mwenyezi Mungu kwa kufuata mambo mema aliyoyafanya Mtume Mohamedi  SW  ili kushiriki ibada pamoja na kufunga kwa ajili ya matendo mema ya Swawabu.
 
 

Maalim Simba alizungumza hayo kwa niaba ya mkuu wa Bagamoyo, Sheikh Abdulqri Ramiya ambapo aliwataka wananchi wa wilaya hiyo na duniani kwa ujumla kwa dini zao kuheshimiana na kupendana ili kuhepukana na migogoro isiyo ya lazima.

Meya wa Bagamoyo ambaye pia ni mwenyekiti wa mji mdogo, Abdul Zohoro Sharifu alisema mwezi huu ni vizuri waumini wakatoa msaada kwa jamii isiyokuwa na uwezo ili kuwasaidia kupatafutari, kwa kuwa nao wanahitaji  funga ya Ramadhani.

Meya huyo alisema yeye binafsi anafata njia za Mtume Mhamedi SW njia zote za Imani ya Kislam,ameanza kutoa vyakula kwa kaya isiyo kuwa na uwezo kimaisha kwa kata 22 kwa jimbo la Bagamoyo,Pia amegawa vitabu  vya Quruani takatifu,Juzuu,Tasibini,Kanzu na Kofia.

Sharifu alisema watanzania waachane na mtazamo mdogo kwa baadhi ya wanasiasa kuwa wanapowasaidia wananchi wasiojiweza au kitu chochote cha maendeleo kuwa unaitaji uongozi mtazamo huo unarudisha nyuma maendeleo ya taifa.

                                  
Share on Google Plus

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment

0 comments:

Inaendeshwa na Blogger.

Wanaofuata

TANGAZO

My Blog List