Na Gloria
Matola
WAVUVI wa
Samaki Wilaya ya Bagamoyo wako katika wakati mgumu wa kimaisha kutokana na
ukosefu wa vifaa vya uvuvi.
Kutokana na
hali hiyo wakazi wengi wa eneo hilo wamejikita katika uvuvi haramu ili kujiinua
kimaisha na kupata kitoweo.
Wavuvi hao
wakizungumza na waandishi wa habari, pembezoni mwa fukwe ya bahari ya Hindi
eneo la Bagamoyo walisema kuwa wanatambua kuwa uvuvi haramu siyo mzuri kutokana
na ukweli kuwa unaua mazalio ya Samaki na kuathiri mikoko.
Mmoja wa
Wavuvi hao, Shaban Kassim alisema kuwa hawapendi kuvua kwa baruti wala nyavu haramu
pamoja na vifaa vinavyoharibu mazalia ya samaki na mikondo ya Bahari lakini
inatokana na hali duni.
Mvuvi
mwingine aliyejitambulisha kwa jina la Ramdhani Swalehe ameiomba serikali kuwa
makini na fedha zinazotolewa kwa ajili ya miradi ya maendeleo kwa jamii na kuhakikisha
inawafikia walengwa.
Alisema
Serikali imekuwa ikijitahidi kutoa pesa kupitia kwenye halmashauri za wilaya
nchini lakini utekelezaji wa miradi hiyo imekuwa ni changamoto kwa jamii nchini
wakiendelea kuishi maisha ya kimasikini chini ya dora moja kwa kaya.
Serikali
pamoja na jitihada za kutokomeza umasikini lakini bado mafanikio kwa wananchi
inatakiwa kuendelea jitihada za makusudi kwa kushirikiana na wadau mbalimbali
wa maendeleo ili kukuza uchumi wananchi.
0 comments:
Chapisha Maoni