Ngorongoro Heroes yawafuta machozi Watanzania



* Waing'oa Kenya kwa mikwaju ya penati
Mchezaji Idd Suleimana Tanzania akichanja mbuga mbele ya wachezaji wa Kenya U20
TIMU ya soka ya taifa ya Vijana U20, Ngorongoro Heroes jioni hii imewafuta machozi Watanzania baada ya kuiodnosha patupu timu ya Kenya kwa kuifunga mkwaju ya penati 4-3 katika mechi ya kuwania kucheza Fainali za Afrika.
Ngorongoro imepata ushindi huo baada ya kushindwa kutambiana na vijana wenzo katika mechi iliyochezwa kwenye uwanja wa Taifa ikiwa ni siku moja tangu kaka zao kunyukwa 3-0 na Burundi katika mechi ya kimataifa ya kirafiki kuadhimisha sherehe za Muungano.
Katika mechi hiyo Tanzania ilipata penati kupitia kwa Kevin Friday, Mohammed Hussein, Mange Chagula na Iddi Suleiman, huku Mudathir Yahya alikosa yake.
Wakenya walipata penati zao kupitia Geofrey Shiveka, Timonah Wanyonyi na Victor Ndinya, huku Evans Makari na Harison Nzivo walipoteza.

Kwa kufuzu huko Tanzania sasa inatarajiwa kuvaana na Nigeria katika hatua inayofuata katika kuwania kucheza fainali hizo zitakazofanyika nchini Senegal.
Share on Google Plus

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment

0 comments:

Inaendeshwa na Blogger.

Wanaofuata

TANGAZO

My Blog List