TRA YAENDELEA NA MAPAMBANO DHIDI YA UMASKINI KWA KUTOA MISAADA YA KUBORESHA MAENDELEO YA JAMII

Mamlaka ya Mapato Tanzania TRA  imetoa msaada wa vifaa mbalimbali vyenye thamani  ya zaidi ya shhilingi milioni arobaini kwa ajili ya kusaidia maendeleo katika jamii.

Vifaa vilivyotolewa ni madawati 100 kwa shule ya msingi Misitu iliyopo kata ya kivule pamoja na vifaa vya usafi katika hospitali ya wilaya ya Temeke.


Kaimu Kamishna Mkuu wa forodha TRA Tiagi Masamaki amesema TRA imetoa msaada huo ikiwa ni muendelezo wa  kuadhimisha wiki ya mlipa kodi.

Naye Muuguzi wa wagonjwa waliolazwa katika Hospitali hiyo  Nurse Nuswe Ambokile   amesema msaada huo umekuja wakati muafaka

Mwalimu Mkuu wa shule ya msingi Misitu Bi Hyasinta  Hugo amesema kumekuwa na changamoto nyingi katika sekta ya Elimu  nchini.

Diwani  Kata ya Kivule  Nyansika Motena na baadhi ya wanafunzi wa shule hiyo wamezungumzia msaada huo.

Mamlaka ya mapato Tanzania TRA inatarajia kuhitimisha ziara zake za wiki ya mlipakodi katika visiwa  vya Zanzibar ambapo pia watafanya shughuli za kijamii.

Displaying DSC01370.JPG

Displaying DSC01345.JPG

Displaying DSC01361.JPG


Share on Google Plus

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment

0 comments:

Inaendeshwa na Blogger.

Wanaofuata

TANGAZO

My Blog List