Hatua inafuatia makubaliano ya mkutano mkuu wa CHADEMA baada ya kujiridhisha kwamba Edward Lowassa ndiye chaguo la Watanzania atakayetimiza ndoto ya upinzani kushika dola.
Mwenyekiti wa CHADEMA Taifa Freeman Mbowe amesema ni lazima kujitoa muhanga ili kutimiza ndoto ya upinzani kuleta mabadiliko bila kujali maslahi binafsi.Pia amegusia suala la ukimya wa Katibu Mkuu wa CHADEMA Dokta Wilbroad Slaa kuwa ni makubaliano apumzike kwa mda lakini nafasi yake ipo palepale.
Aliyekuwa Mwenyekiti wa wenyeviti wa Mikoa CCM,mgana Msindai aliyejiunga na CHADEMA ameelezea sababu za kujiengua na CCM huku Mwenyekiti mwenza wa UKAWA na Mwenyekiti wa NCCR Mageuzi James Mbatia akielezea uteuzi wa Lowassa ndo suluhu ya UKAWA kushika Dola.
0 comments:
Chapisha Maoni