SERIKALI YAJIPANGA KUSIMAMIA MAADILI NA KANUNI ZILIZOPANGWA.

Seriakali imejipanga kuboresha sekta ya wahasibu ili kuhakikisha maadili mema ya kazi,kanuni na sheria ndogo kwa wahasibu zinafuatwa huku taaluma hiyo ikizidi kuongeza idadi kubwa ya watu wanaoingia katika sekta hiyo.

Rai hiyo imetolewa wakati wa mahafali ya Wahitimu wa chuo cha NBAA nje kidogo ya jiji la Dar es salaam amabao waliaswa kutumia vyema taaluma yao.Jumla ya wahitimu 1,058walihitimu katika mahafali hayo ya 37.

Hayo yamesemwa na Waziri wa nchi Ofisi ya Rais asiyekuwa na wizara maalum,Profesa Mark Mwandosya aliyekuwa mgeni rasmi amesema Serikali lazima iangalie suala la maadili kwa wanataaluma wa ndani wa mahesabu ili kuepusha tatizo la ufisadi.

Naye Prof Isaya JAIRO,Mwenyekiti wa Bodi ya NBAA na mkurugenzi mtendaji wa bodi Pius Maneno kwa pamoja wametoa wito wa wahitimu hao kulinda na kukuza rasilimali zilizopo za Taifa.Nao baadhi ya wahitimu wameimba Serikali iwatumie wataalam wa ndani ili kukuza vipaji vya wazawa wa ndani katika suala la mahesabu.
Share on Google Plus

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment

0 comments:

Inaendeshwa na Blogger.

Wanaofuata

TANGAZO

My Blog List