Mkurugenzi Mtendaji wa Tume ya Kudhibiti Maambukizi ya Ukimwi, Dkt Fatma Mrisho amesema tatizo la Ukimwi bado ni kubwa kwa Vijana hali inayochangiwa na kufanya ngono zembe. Dkt Fatma amesema katika ukuaji wa tatizo hilo, Vijana wa Kike ndiyo wanaongoza kwa Maambukizi hayo ikilinganishwa na wale wa Kiume. hayo ameyasema wakati wa kufunga Semina ya Vijana kuhusu Ukimwi pamoja na Maambukizi ya VVU. James Kajingwa Mkurugenzi wa Maendeleo ya Vijana nchini amewataka Vijana wajiepushe na Utumiaji wa Ulevi wa kupitiliza unaweza kuchochea tabia ya kufanya ngono zembe na kupelekea Maambukizi ya UVV, pia amewataka Vijana kujitambua sambamba kuwa Mabalozi wa wengine kwa ajili ya kulinda vizazi vijayo kwa kutoa elimu ya mapambano dhidi ya Maambukizi ya VVU
WAZIRI MASAUNI ZIARANI OSLO NORWAY
-
Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais Muungano na Mazingira Mhe.Hamad
Masauni ameongoza ujumbe wa Tanzania kutembelea Kampuni ya Hafslund
Celsion inay...
Saa 20 zilizopita
0 comments:
Chapisha Maoni