USAFI TEMEKE GEREJI BUBU BASI MAFICHO YA WAHALIFU

Serikali imejipanga kuwakamata wale wote wenye Gereji Bubu kwenye makazi ya Watu Kutokana na Watu  wahalifu kufanya maficho yao, na kuchangia kuharibu hali ya usafi wa Mazingira, Hayo yamesemwa katika usafi wa Wilaya ya Temeke ukiwashirikisha wadau mbalimbali wakiwepo Jeshi la Wananchi Tanzania, Askari Polisi, Wasanii mbalimbali, Wananchi na wanafunzi. Mkuu wa Wilaya ya Temeke Felix Lyaniva ametowa onyo watu wenye Gereji Bubu waende kuzisajiri ili wapate maeneo rasmi ya kufanyia kazi za Gereji. Brigedia Jenerali Domonic Mrope Mkuu wa kamandi Vikosi chini ya Makao ya Jeshi  GOC amesema kazi ya usafi ni moja wapo ya Kazi za Kijamii wanazifanya kwa kushirikiana na Wananchi pamoja na huduma mbalimbali za Kijamii wakifanya hivyo  kutoa huduma hadi tar. 1 9. 2016 Jeshi la Wananchi wakitimiza miaka 52

Share on Google Plus

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment

0 comments:

Inaendeshwa na Blogger.

Wanaofuata

TANGAZO

My Blog List