Baraza la kuu la Uongozi la Chama cha wananchi CUF limeiagiza kamati ya maadili na nidhamu kumuhoji katibu mkuu wa chama hicho Maalim Seif Sharif Hamad kwa madai ya kuhusika na njama ya kukihujumu chama hicho.
Hayo yamesemwa na Mwenyekiti wa chama cha CUF Profesa Lipumba katika juhudi zake za kuimarisha chama cha CUF ambapo karibuni kimeonekana kuyumba na kutawaliwa na migogoro. Profesa Lipumba amesema katiba na sheria zilizounda bodi ya wadahamini CUF na halali hivyo kupingana na juhudi hizo ni hujuma dhidi ya Chama cha CUF.
Pia amesema Maalim Seif Sharif Hamad hana uwezo wa kupinga au kufungua kesi dhidi ya bodi ya wadahamini ya Chama cha wananchi CUF.
Mapema chama cha CUF kilichagua bodi ya wadahamini kupitia baraza kuu la Chama hicho na kupishwa na kusajiliwa rasmi. Lakini bodi hiyo ilipingwa vikali na Katibu mkuu wa chama hicho Maalim Seif Sharif Hamad kwa madai inataka kumtoa kwenye nafasi yake na kuwakosesha haki Wana CUF.
BALOZI MUSSA AKAGUA MAJENGO YA UBALOZI WA TANZANIA NCHINI MALAWI.
-
Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki
ambaye pia ni Mwenyekiti wa kamati ya miradi ya Wizara, Balozi Said Shaib ...
Saa 13 zilizopita
0 comments:
Chapisha Maoni