Baraza la kitaifa la michezo nchini Tanzania limevunjwa kufuatia madai ya ufisadi.
Hatua hiyo inajiri wiki mbili tu baada ya maafisa wakuu wa shirikisho la soka nchini humo kushtakiwa na ulanguzi wa fedha.
Kulingana na mwandishi wa BBC Sammy Awami hatua hiyo ilitarajiwa.
Baraza hilo ambalo linahusika na usimamizi wa michezo nchini humo limetuhumiwa kwa kukosa utendaji.
Akilifutilia mbali baraza hilo, waziri wa michezo Harrison Mwakyembe alisema kuwa kushindwa kwao kuimarisha michezo nchini hakutokani na uhaba wa fedha bali uzembe na kutoijali sekta hiyo.
Pia ameshutumu operesheni za baraza hilo kwa kutawaliwa na ufisadi, madai ambayo aliyekuwa katibu mkuu wa baraza hilo Mohammed Kiganja ameyakana.
"kwanza nataka kusema kwamba hakujakuwa na ufisadi katika baraza hilo.Ufisadi umeshamiri katika michezo kwa jumla. Na ninakubaliana na hilo.Iwapo utaenda katika uchaguzi wa vilabu vya soka kuanzia viwango vya Wilaya hadi kitaifa utaona matatizo haya''.
Kuvunjwa kwa baraza hilo kunajiri wiki mbili tu baada ya rais na maafisa wengine wakuu wa shirikisho la soka kushtakiwa kwa ulanguzi wa fedha.
BONDIA RAMADHANI MIGWENE AMUWEKEA MIKWALA ALBANO CLEMENT BAADA YA KUKIMBIWA
NA HABIBU PENGO
-
BONDIA RAMADHANI MIGWEDE baada ya kukimbiwa na mpinzani wake Habibu Pengo
aliesaini nae kuzipiga mara ya kwanza sasa amebadilishiwa mpinzani na
atache...
Miaka 2 iliyopita
0 comments:
Chapisha Maoni