Mheshimiwa Diwani Nuru Awadhi wa viti maalamu wa Wilaya ya Ilala ambaye anawakilisha kundi la watu wenye ulemavu ametoa msaada kwa watoto wa madrasa.

Mheshimiwa Diwani NURU AWADHI wa viti maalamu wa Wilaya ya Ilala ambaye anawakilisha kundi la watu wenye ulemavu ametoa msaada kwa kwa watoto wenye ulemavu na wazima kwa ajili ya kujifunza elimu ya dini ya Kiislamu. Mheshimiwa Diwani Nuru ametoa msaada vitabu dini ya Kiislamu na Mashine kwa ajili kuandika na kujifunza kwa watu wenye ulemavu wa macho.

Mheshimiwa Diwani Nuru Awadhi alifuatana na Mwenyekiti wa Buguruni ambaye kwa pamoja wamesema serikali imetenga bajeti kwa ajili ya makundi maalum lakini juhudi za viongozi ni chachu za kufanikisha malengo ya kugusa hayo makundi maalum na kutolea mfano kwa Diwani wa viti maalamu Nuru jinsi alivyopigana kupata vifaa hivyo.

Kwa niaba ya wanafunzi wa wanufaikaji wa msaada huo aliongea kutoa shukrani kwa Mheshimiwa Diwani Nuru Awadhi ambaye alisema pia aliwahi kuwa mwanafunzi wake kipindi cha chuma.

Vifaa hivyo alivyotoa Diwani Nuru baadhi alitoa ela zake mwenyewe na baadhi kuomba msaada kwa marafiki  zake waishiyo afrika kusini.  ukiwepo na ubao wa kufundishia, Vitabu na Mwisho amewataka walimu na wanafunzi kutumia msaada waliopata wa vifaa hivyo vizuri ili waweze kuwa mabolozi wazuri baadaye. 

Share on Google Plus

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment

0 comments:

Inaendeshwa na Blogger.

Wanaofuata

TANGAZO

My Blog List