Neymar asilimia 90 kuondoka Barcelona
Uwezekano wa mshambuliaji raia wa Brazil Neymar Jr kuondoka katika klabu ya Barcelona ni mkubwa kutokana na mchezaji huyo kutokuwa na furaha ndani ya klabu hiyo.
Kuna taarifa kuwa mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 25 anataka kucheza katika klabu nyingine ili aweze kung’ara na kushinda Ballon d’Or kitu ambacho hawezi kufanya Barcelona kutokana na uwepo wa Lionel Messi.
Klabu ya Paris Saint-Germain ndio klabu pekee iliyo tayari kutoa kiasi kikubwa cha pesa ambayo Barcelona wanaitaka ili kumnunua Neymar huku klabu za Chelsea na Manchester United zikiwa haziko tayari kufanya hivyo.
PSG ambao wamekuwa wakimtaka Neymar kwa kipindi kirefu sasa wako tayari kutoa kiasi cha pauni milioni 196 ili kumsajili mshambuliaji huyo.
Taarifa zinasema Barcelona wamekuwa wakimtaka Neymar kukana kwa Uma taarifa za kuwa hana furaha katika klabu hiyo lakini mchezaji huyo hajafanya hivyo.
Upo uwezekano wa Neymar kuondoka Barcelona na kuna taarifa kuwa amewaambia rafiki zake wa karibu jambo hilo.
Wakati huohuo raisi wa klabu ya Barcelona Josep Bartomeu amesema Neymar hauzwi.
MWENGE WA UHURU WAWAVUTIA WATALII NGORONGORO
-
Na Mwandishi wetu Ngorongoro.
Baadhi ya watalii waliokuwa katika safari zao za kawaida kwenye eneo la
hifadhi ya Ngorongoro leo jumatano tarehe 9 Julai...
Saa 7 zilizopita
0 comments:
Chapisha Maoni